Skip to main content

Posts

NENO LA MUNGU

KUTOKA 6 ;6-7          6 Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa; 7 nami nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ni YEHOVA, Mungu wenu, niwatoaye mtoke chini ya mizigo ya Wamisri. MATHAYO 15;30-31          30 Wakamwendea makutano mengi wakimletea viwete, vipofu, mabubu, vilema, na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; akawaponya; 31 hata ule mkutano wakastaajabu, walipowaona mabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanakwenda, na vipofu wanaona; wakamtukuza Mungu wa Israeli.
Recent posts

MAANDALIZI YA KUFANIKISHA SHEREHE YA UPADRISHO WA BWANA JOSEPHAT OROTA

KWA HESHIMA NA SHUKRANI KWA MUNGU, FAMILIA YA BW. NA BIBI PAUL MBIWI OROTA WA UCHAU KIBOSHO, WANAYO FURAHA KUKUJULISHA/KUWAJULISHA KUWA KIJANA WAO MPENDWA SHEMASI JOSEPHAT MSAKURE OROTA ANATARAJIA KUPEWA DARAJA TAKATIFU LA UPADRI TAR 06.07.2017. HIVYO UKIWA KAMA NDUGU WA KARIBU WA FAMILIA HII UNAOMBWA KUSHIRIKIANA NAO KATIKA MAANDALIZI YA KUFANIKISHA SHEREHE HII MUHIMU YA UPADRISHO NA MISA YAKE YA SHUKRANI. KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA DADA YAKE, RENALDA OROTA 0756 315 726

KATIBA YA UMOJA WA VIJANA WA UKOO WA OROTA (UVUO)

UTANGULIZI Kikundi cha UMOJA WA VIJANA WA UKOO WA OROTA (UVUO)  kimeazishwa rasmi Oktoba 2016, kikundi hiki si cha kibiashara na kimeundwa kwa mudhumuni ya kuwaleta pamoja Vijana wa Ukoo wa Orota ili kudumisha UNDUGU NA MSHIKAMANO wetu na kukua kama familia moja yenye kupendana na kumcha Mungu. Taratibu za kikundi hiki cha UVUO zimeandikwa katika katiba hii na ndizo zitakazotumika kama mwongozo wa kikundi katika mambo yote yahusuyo uendeshaji wa kikundi. Katiba hii imepitishwa kwa kauli moja na wanachama waanzilishi na kila mwanachama atakayejiunga na kikundi atawajibika kuisoma katiba hii, kuielewa na kuitetea. 1.       TARATIBU ZA KIKUNDI 1.1.             JINA LA KIKUNDI NA MAKAO MAKUU (a)    Jina la Kikundi litakuwa “UMOJA WA VIJANA WA UKOO WA OROTA” (UVUO) (b)    Makao makuu ya Kikundi yapo Moshi, Kilimanjaro.. (    c)    Muhuri wa Kikundi utakuwa na maneno UVUO 1.2.             MADHUMUNI (a)    Kuwaunganisha pamo