Skip to main content

KATIBA YA UMOJA WA VIJANA WA UKOO WA OROTA (UVUO)

UTANGULIZI

Kikundi cha UMOJA WA VIJANA WA UKOO WA OROTA (UVUO)  kimeazishwa rasmi Oktoba 2016, kikundi hiki si cha kibiashara na kimeundwa kwa mudhumuni ya kuwaleta pamoja Vijana wa Ukoo wa Orota ili kudumisha UNDUGU NA MSHIKAMANO wetu na kukua kama familia moja yenye kupendana na kumcha Mungu.
Taratibu za kikundi hiki cha UVUO zimeandikwa katika katiba hii na ndizo zitakazotumika kama mwongozo wa kikundi katika mambo yote yahusuyo uendeshaji wa kikundi.
Katiba hii imepitishwa kwa kauli moja na wanachama waanzilishi na kila mwanachama atakayejiunga na kikundi atawajibika kuisoma katiba hii, kuielewa na kuitetea.

1.      TARATIBU ZA KIKUNDI

1.1.            JINA LA KIKUNDI NA MAKAO MAKUU

(a)   Jina la Kikundi litakuwa “UMOJA WA VIJANA WA UKOO WA OROTA” (UVUO)
(b)   Makao makuu ya Kikundi yapo Moshi, Kilimanjaro..
(    c)   Muhuri wa Kikundi utakuwa na maneno UVUO

1.2.            MADHUMUNI

(a)   Kuwaunganisha pamoja Vijana wa Ukoo wa Orota kutoka mashinani hadi mijin.
(b)  Kuwaleta pamoja Vijana wa Ukoo wa Orota ili kufahamiana na kuweza kuendeleza desturi na mila nzuri za Ukoo wa Orota ikiwa ni pamoja na kusaidiana wakati wa shida na raha.
(c)   Kuanzisha mfuko wa UVUO ambao unaweza kusaidia katika maendeleo ya familia zetu hasa katika swala zima la elimu, tafrija, mazishi na ujasiriamali kuendana na kanuni za katiba.
(d)  Kuanzisha miradi ya maendeleo yenye lengo la kuhakisha kikundi kina uwezo wa kutekeleza shughuli zake.

2.      UANACHAMA

(a)          Kutakuwa na wanachama wa aina mbili, yaani, Wanachama Waanzilishi na Wanachama Washiriki.
(b)         Mtu yeyote mwenye umri wa kuanzia miaka 18 na kuendelea anaweza kuomba uanachama katika kikundi hiki iwapo anazo sifa stahili za kujuinga na kikundi kama zilivyoainishwa katika katiba hii.
(c)          Wanachama washiriki watachaguliwa na kufanywa wanachama baada ya kujaza fomu maalum ya maombi, na maombi yao kupendekezwa na wanachama waanzilishi wasiopoungua wawili.
(d)         Kwamba maombi yote ya kujiunga na kikundi yatajadiliwa katika Mkutano Mkuu (au mkutano wa wanachama ulioitishwa kwa ajili hiyo) wa kikundi, na yatakubaliwa kwa kura. Ili mtu aweze kuwa mwanachama atatakiwa kukubaliwa na wanachama wasiopungua asilimia  hamsini katika mkutano halali wa kikundi.
(e)          Sifa za Uanachama
(i)             Isipokuwa kwa wanachama waanzilishi wa kikundi hiki ambao kwa kutia saini katiba hii tayari wanafahamu malengo ya kikundi hiki, mtu yeyote mwenye umri kuanzia miaka 18 na kuendelea ambaye Ukoo wake ni OROTA na aliyesoma na kuelewa katiba hii anaweza kuomba kuwa mwanachama wa Kikundi hiki.
(ii)           Mwanachama anatakiwa kuwa tayari kufanya kazi za kikundi kwa kujitolea na kuhakikisha kuwa anakuwa wa mchango mkubwa katika kukamilisha madhumuni ya kikundi hiki.

2.1.            MASHARTI YA UANACHAMA

(a)   Kiingilio: Ili kuwa mwanachama kila mwanachama aliyepitishwa na Mkutano anapaswa kulipa kiasi cha shilingi 10,000/=. Kiasi hiki cha fedha chaweza kulipwa kwa mkupuo mmoja au kwa awamu ndani ya miezi mitatu ya kwanza.
(b)   Ada: kila mwanachama anapaswa kulipa ada ya kila mwezi kiasi cha shilingi 3,000/= (36,000/= kwa Mwaka). Mwanachama atakayeshindwa kulipa ada ya mwezi kwa miezi mitatu mfululizo atakuwa amejivua uanachama na iwapo atataka kurudi itambidi alipe faini ya shilingi 20,000/= pamoja na malimbikizo ya miezi yote mitatu.
(c)   Malipo yote yatafanywa kwa Mweka Hazina na atatakiwa kutoa risiti kwa kila malipo atakayopokea.
(d)   Mweka hazina atawajibika kuweka fedha katika acunt ya bank kwaajili ya kikundi.
(e)   Kila anayetaka kujiunga na kikundi ni lazima apewe nakala ya katiba ambayo ataisoma na akikubaliana na taratibu zote itabidi asaini fomu maalum kama ushahidi kuwa anakubaliana na masharti yote ya kikundi na yuko tayari kuwa mwanachama.

2.2.            HAKI NA WAJIBU WA MWANACHAMA

(a)   Kila mwanachana ana haki ya kutoa mawazo yake bila woga hata kama mawazo hayo yatapingana na kiongozi yoyote au mwanachama mwingine.
(b)   Kila mwanachama ana haki ya kupiga kura kuchagua viongozi au kugombea nafasi yoyote ya uongozi kwa mujibu wa katiba.
(c)   Kila mwanachama ana wajibika kuhudhuria katika shughuli zote zinazohusu kikundi na wanachama wenzake bila ubaguzi.
(d)   Kila mwanachama ana wajibu wa kusoma na kuielewa vyema katiba ya Kikundi na kufuata maelekezo yake. Atakayekwenda kinyume kwa makusudi  atahesabiwa kuwa ni msaliti wa kikundi na hatua dhidi yake zitachukuliwa ikiwepo kupewa onyo au kufukuzwa uanachama.

2.3.            KUPOTEZA UANACHAMA

Mwanachama anapoteza haki yake ya kuwa mwanachama kutokana na sababu zifuatazo:
(i)                 Kifo
(ii)              Kutohudhuria vikao vya kikundi bila taarifa yoyote kwa MIAKA MITATU mfululizo au kubainika kuwa sababu zinazotolewa na kutohudhuria vikao siyo za msingi.
(iii)            Kushindwa kutimiza masharti ya katiba,
(iv)            Kujiuzulu
(v)              Kutowakilisha michango ya mwezi kwa miezi mitatu mfululizo.
(vi)            Ikidhibitika kwamba mwanachama ana tabia za uchochezi zinazovuruga amani baina ya wanachama.
(vii)          Kufanya kazi binafsi kwa kutumia jina la kikundi bila kikundi kuwa na taarifa.
(viii)       Ikiwa italetwa mada na mwanachama/ kikundi ya kumfukuza mwanachama uanachama kwa sababu ya kushindwa kutimiza masharti ya katiba au uchochezi. Mleta mada atatakiwa kupeleka kwa maandishi sababu za mada yake na mwanachama anayetuhumiwa atapewa nafasi ya utetetezi wa maandishi. Maumuzi yote yatatakiwa kufanywa katika mkutano mkuu kwa kura zisizopungua theLuthi mbili ya wanachama waliohudhuria.
(ix)            Endapo mwanachama atapoteza haki yake ya uanachama, kiingilio na michango aliyotoa havitarudishwa.

3.      VIONGOZI

3.1.            KAMATI KUU

Kikundi kitakuwa na viongozi wa kamati kuu wafuatao:
(a)   Mwenyekiti; Josephat Orota
(b)  Makamu Mwenyekiti; Renalda Orota
(c)   Katibu; Agnes Patrick Orota
(d)  Katibu Msaidizi; Joseph Remi Orota
(e)   Mweka Hazina: Agnes Martini Orota (mweka sahihi bank)
(f)    Mweka Hazina Msaidizi

3.2.            KAMATI YA NIDHAMU (NA MATUKIO)

Kikundi pia kitakuwa na viongozi wa kamati ya Nidhamu na Matukio ambao ni:
(a)   Mwenyekiti: Josephat Orota
(b)   Makamu Mwenyekiti: Renalda Orota
(c)   Katibu:  Agnes Patrick Orota
(d)   Katibu msaidizi: Joseph Remi Orota
(e)   Pascal Orota
(f)    Rose Patrick Orota (Mweka sahihi bank)
(g)   Cosmas Peter Orota
(h)   Leon Orota
(i)     Rodrigers Orota
v  Nafasi za uongozi zilizotajwa hapo juu zitajazwa kwa wagombea kuchaguliwa na wanachama kwenye mkutano mkuu utakaohudhuriwa na theluthi mbili ya wanachama hai.
v  Kipindi cha uongozi kitakuwa cha muda wa MIAKA MIWILI mpaka hapo itakapoamuliwa vingine.
v  Uchaguzi mdogo unaweza kufanyika iwapo kiongozi atapoteza haki yake ya kuwa mwanachama.
v  Ili mwanachama aweze kugombea au kuchaguliwa kushika nafasi yoyote ya uongozi ni lazima awe amemaliza kulipa kiingilio na ada na amedumu ndani ya chama kwa kipindi kisichopungua mwaka Mmoja  ili awe amefahamika vizuri na wanachama wengine.

4.      VIKAO

v  Mambo yafuatayo yatazingatiwa kuhusu vikao.

4.1.            AINA ZA VIKAO

v  Kikundi kitakuwa na vikao vya aina tatu;
(i)                 Kikao cha kila mwezi ambacho kitajadili maendeleo ya kikundi, kuidhinisha wanachama wapya na kupeana taarifa ya mambo mbalimbali katika kujiendeleza. Kikao hiki kitafanyika kila JUMAPILI ya mwanzo wa mwezi saa kumi na moja jioni (11:00) kwa njia ya mtandao wa WHATSAPP.
(ii)              Vikao vya kila wiki kwa viongozi wote wa kikundi kujadili namna ya uongozi bora wa kikundi changamoto mbalimbali za wanachama.
(iii)            Mkutano mkuu ambao utafanyika kila baada ya mwaka mmoja. Kikao hiki kitaangalia mafanikio na matatizo na ndicho kitahusika na uchaguzi wa viongozi pale viongozi wanapokuwa wamemaliza muda wao. Kikao hiki lazima kihudhuriwe na wanachama wasiopungua theluthi mbili ya wanachama hai. Wanachama hai ni wale waliolipia vizuri ada zao na wanaohudhuria mikutano/vikao vya kikundi.
(iv)            Kikao cha dharura ambacho kitaitishwa na katibu wa kamati ya nidhamu na matukio na kuendeshwa na mwenyekiti wa kamati ya nidhamu na matukio.

4.2.            TARATIBU ZA VIKAO

(i)                 Mwenyekiti au Makamu Mwenyekiti ndiye atakayeendesha vikao akisaidiana na Katibu atakayechukua kumbukumbu zote za vikao.
(ii)              Kiongozi yoyote anayo wajibu wakumbusha au kumuuliza katibu mda wa kikao.
(iii)            Kikao kitajadili mada zitakazowasilishwa na ikiwa kutatokea mvutano, basi kura ya siri/wazi itatoa uamuzi na kama baada ya kupiga kura matokeo yatakuwa sawa uamuzi utatolewa na mwenyekiti kwa kupiga kura ya turufu.
(iv)            Maamuzi yatakayoamuliwa na theluthi mbili ya wanachama yamepitishwa.
(v)              Mwanachama ambaye hatahudhuria kikao kwa sababu yoyote ile anatakiwa kutoa taarifa kwa katibu. Udhuru uwe kwa maana halisi ya udhuru na siyo kwa nia ya kukwepa kikao.

5.      FEDHA ZA KIKUNDI

Katika maswala ya fedha kutakuwa na taratibu kwa upande wa makusanyo (mapato) na matumizi ya fedha za mapato. Taratibu hizi zitakubaliwa katika Mkutano Mkuu wa Kikundi.

5.1.             MAPATO

Mapato ya kikundi yatatokana na;
(a)   michango ya wanachama itakayotolewa kama kiingilio, ada ya mwezi na michango mbalimbali kutoka kwa wanachama pale inapobidi.
(b)  Misaada kutoka kwa wahisani na wafadhili. (ndani na nje ya nchi)
(c)   Miradi mbalimbali itakayobuniwa na wanachama katika kuhakikisha kuna ustawi wa kikundi kwa ajili ya kutekeleza madhumuni ya kikundi.

5.2.            MATUMIZI YA MAPATO

(a)   Mapato yote ya kikundi yatatumika kwa ajili ya kutekeleza madhumuni ya kikundi.
(b)   Kikundi kitatumia mapato yake kwa ajili ya kusaidia wanachama pamoja na kuchangia misiba au sherehe kwa wanachama wake.
(c)   Hakutakuwa na mikopo kutoka kwenye mfuko wa kikundi na fedha za kikundi zitatumika kwaajili ya kusaiaidia wanachama kama ilivyo ainishwa hapo juu (ab).

6.      MENGINEYO

(a)   Wanachama katika Mkutano Mkuu wanaweza kuamua kwa kura zisizopungua asilimia tisini (90%) wa wanachama hai walioshiriki kufanya marekebisho ya katiba hii. Taarifa ya marekebisho na aina ya marekebisho lazima itolewa na Mwenyekiti kwa wanachama hai wote siku thelathini (30) kabla ya kikao kinachotarajiwa kujadili marekebisho ya Katiba.
(b)  Mkutano Mkuu wa kikundi waweza kuamua kusitisha shughuli za Kikundi hiki kwa kura zisizopungua asilimia tisini (90%) za wanachama hai. Taarifa ya chini ya kifungu hiki lazima itolewe na Mwenyekiti kwa wanachama hai wote siku thelathini (30) kabla ya kikao. Iwapo Huduma ya Kikundi hiki itasitishwa basi mali zote za kikundi zitahamishiwa kwa kikundi cha UKOO WA OROTA.
(c)   Mali zote za Kikundi zitakuwa chini ya jina la kikundi na zitakuwa chini ya uongozi wa Kikundi ambao muda wote utatunza kumbukumbu za mali zinazomilikiwa na kikundi.
(d)  Katika upanuzi wa shughuli zake, kwa makubaliano katika Mkutano Mkuu, kikundi chaweza kujisajilii chini ya sheria yoyote husika ili kuleta ufanisi katika kutekeleza madhumuni yake.

(e)   Mwanachama yoyote mwenye malalamiko katika utekelezaji wa shughuli za Kikundi aweza kuyawasilisha kwa Mwenyekiti ambaye atayafikisha katika Kamati Kuu ambayo itayajadili na kutayatolea ufafanuzi.

Comments

  1. Hongereni kwa katiba nzuri ndg zanguni akina Orota wa kibosho

    ReplyDelete
  2. Wakuu mko vizur pia asante kwakunipa somo maana nimepewa jukumu la kuandaa kama hiyo pia .

    ReplyDelete
  3. Congratulations Orota Family Kwa katiba nzuri

    ReplyDelete
  4. Vizuri sana orota family

    ReplyDelete

Post a Comment

Popular posts from this blog

MAANDALIZI YA KUFANIKISHA SHEREHE YA UPADRISHO WA BWANA JOSEPHAT OROTA

KWA HESHIMA NA SHUKRANI KWA MUNGU, FAMILIA YA BW. NA BIBI PAUL MBIWI OROTA WA UCHAU KIBOSHO, WANAYO FURAHA KUKUJULISHA/KUWAJULISHA KUWA KIJANA WAO MPENDWA SHEMASI JOSEPHAT MSAKURE OROTA ANATARAJIA KUPEWA DARAJA TAKATIFU LA UPADRI TAR 06.07.2017. HIVYO UKIWA KAMA NDUGU WA KARIBU WA FAMILIA HII UNAOMBWA KUSHIRIKIANA NAO KATIKA MAANDALIZI YA KUFANIKISHA SHEREHE HII MUHIMU YA UPADRISHO NA MISA YAKE YA SHUKRANI. KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA DADA YAKE, RENALDA OROTA 0756 315 726

NENO LA MUNGU

KUTOKA 6 ;6-7          6 Basi waambie wana wa Israeli, Mimi ni YEHOVA, nami nitawatoa ninyi mtoke chini ya mizigo ya Wamisri, nami nitawaokoa na utumwa wao, nami nitawakomboa kwa mkono ulionyoshwa, na kwa hukumu kubwa; 7 nami nitawatwaeni kuwa watu wangu, nitakuwa Mungu kwenu; nanyi mtajua ya kuwa mimi ni YEHOVA, Mungu wenu, niwatoaye mtoke chini ya mizigo ya Wamisri. MATHAYO 15;30-31          30 Wakamwendea makutano mengi wakimletea viwete, vipofu, mabubu, vilema, na wengine wengi, wakawaweka miguuni pake; akawaponya; 31 hata ule mkutano wakastaajabu, walipowaona mabubu wanasema, vilema wanakuwa wazima, viwete wanakwenda, na vipofu wanaona; wakamtukuza Mungu wa Israeli.